Msajili wa Vyama vya Siasa Anasukumwa Wanataka Kuifuta Chadema- Mnyika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msajili wa Vyama vya Siasa Anasukumwa Wanataka Kuifuta Chadema- Mnyika
Naibu Katibu Kuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bara Mhe. John Mnyika amefunguka na kusema kuwa kuna kila dalili serikali kupitia kwa msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mtungi.


Mnyika akiongea na waandishi wa habari leo Februari 23, 2018 amesema kuwa kuna njama ambazo zinapangwa kuhakikisha kuwa chama hicho kinafutiwa usajili wake jambo ambalo Mnyika anasema jambo hilo hawataliweza.

"Msajili wa vyama vya siasa anasukumwa , dhamira yao ni kutafuta mwanya wa kukifuta Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jambo hili hawaliwezi na kama wanafikiri wanauwezo wa kuifuta CHADEMA wajaribu kufanya hivyo. Wafahamu kwamba wakizuia mlango wa demokrasia, watu watafanya siasa kwa njia nyingine, sisi tutakabiliana na msajili kwa njia yoyote kuhakikisha jambo hili halifanikiwi" alisema Mnyika

Aidha Mnyika amesema kuwa Msajili wa vyama vya siasa nchini amekitaka chama cha Demokrasia na Maendeleo kujieleza kutokana na matukio ya Februari 16, 2018 hivyo amedai tayari wameshamjibu msajili huyo wa vyama vya siasa.

Mbali na hilo Mnyika amewataka wanachama wa CHADEMA pamoja na viongozi wake wakiwepo madiwani pamoja na wabunge wajilinde sana katika kipindi hiki kwani amedai kwa sasa wanashambuliwa kila kona kwa njia mbalimbali.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad