Mwanamume Atolewa Uvimbe wa Kilo 1.8 Kwenye Ubongo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanamume atolewa uvimbe wa kilo 1.8 kwenye ubongo
Madaktari nchini India wamefanya upasuaji wa kipekee na kuondoa uvumbe wa uzani wa kilo 1.8 kutoka kwa mwanamume wa umri wa miaka 31.

Wanasema huo huenda ukawa uvimbe mkubwa zaidi kuwahi kutolewa kwenye ubongo wa binadamu.

Upasuaji huo, ambao ulidumu saa saba, ulifanyika mnamo 14 Februari katika hospitali ya Nair mjini Mumbai magharibi mwa nchi hiyo.

Lakini taarifa za upasuaji huo hazikutangazwa moja kwa moja kwa sababu madaktari hawakuwa na uhakika iwapo ulifanikiwa.

"Sasa ni suala tu lake kupona, lakini maisha yake hayamo hatarini tena," Dkt Trimurti Nadkarni, mkuu wa upasuaji wa mfumo wa neva, ameambia BBC.

Santlal Pal, mwuzaji duka kutoka jimbo la Uttar Pradesh kaskazini mwa India, amekuwa akiishi na uvimbe huo kwa miaka mitatu.

Madaktari wanasema Pal alipoteza uwezo wake wa kuona kutokana na uvimbe huo.

Hata hivyo, kuna matumaini kwamba huenda akapata uwezo wa kuona tena baada ya kupona.

Mke wake ameambia gazeti moja India kwamba alikuwa ameambiwa na madaktari katika hospitali tatu tofauti Uttar Pradesh kwamba uvimbe huo hauwezo kuondolewa.

"Visa kama hivyo huwa hatari sana," Dkt Nadkarni alisema, na kuongeza kwamba Pal alihitaji painti 11 za damu wakati wa upasuaji huo.

Mwanamke aliyetajwa kuwa mwenye uzani mkubwa zaidi duniani amefariki
Aidha, alitumia mtambo wa kumsaidia kupumua kwa siku kadha baada ya upasuaji huo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad