AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
NEC imesema maandalizi hayo ni pamoja na ufumbuzi wa changamoto ndogondogo zinazojitokeza.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima amesema hayo baada ya mkutano wa watendaji wa Tume na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kinondoni, Aron Kagurumujuri.
Kailima amesema Tume inafuatilia kwa karibu maandalizi ya uchaguzi huo utakaofanyika Jumamosi Februari 17,2018.
Katika taarifa ya NEC iliyotolewa leo Februari 11,2018 Kailima amepongeza jitihada zinazofanywa na msimamizi wa uchaguzi na wasaidizi wake katika kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinapatiwa ufumbuzi wa haraka.
Amewashauri wasimamizi wa uchaguzi kuendelea kukutana na wawakilishi wa vyama vya siasa kwa ajili ya kutoa taarifa katika kila hatua.
Kailima amesema Tume imejipanga kuanza kutoa vipindi vya elimu ya mpiga kura mfululizo hadi siku ya uchaguzi.
Amesema elimu itahusu mada kadhaa zikiwemo haki na wajibu wa mpiga kura, wakala wa vyama vya siasa na msimamizi wa uchaguzi pamoja na taratibu zote za upigaji kura.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK