Madaktari Kenya Wasimamishwa Kazi Baada ya Kumfanyia Upasuaji wa Kichwa kwa Mgonjwa Asiyestahili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Madaktari Kenya Wasimamishwa Kazi Baada ya Kumfanyia Upasuaji wa Kichwa kwa Mgonjwa Asiyestahili
Madaktari Hospitali ya Kenyatta wasimamishwa kazi kwa kufanya upasuaji wa kichwa kwa mgonjwa asiyestahili.

Taarifa kutoka mkurugenzi mkuu wa hospitali hiyo, Lily Tare, zinabainisha kuwa wagonjwa wawili waliokuwa hawajitambui na mmoja kati yao ndiye alihitaji upasuaji wa kichwa ili kuondoa damu ilionekana imeviria.

Madaktari Tanzania wafanya upasuaji wa kihistoria
Wanawake waandamana kuhusu madai ya ubakaji katika hospitali Kenya
Lakini pia mkurugenzi huyo ameomba radhi na kusema "tunafurahi kuwatangazia umma kwamba mgonjwa huyo sasa ametibiwa na anaenedelea vizuri"

Wafanyakazi wanaochunguzwa katika sakata hilo ni pamoja na daktari wa upusuaji wa ubongo, muuguzi, mtalaam wa dawa za usingizi.

Hili sio sakata la kwanza kukumba hospitali hiyo, mwezi wa kwanza mwaka huu, waziri wa afya nchini Kenya Dkt Cleopha Mailu aliamrisha uchunguzi ufanyike baada ya wanawake waliojifungua kudai kwamba wanadhalilishwa kingono.

Taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao zilidai kina mama waliojifungua wamekuwa wanashambuliwa na baadhi ya wafanyikazi wakati wakienda kwenye chumba cha watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao.

Tukio hilo liliibua maandamano na wanaharakati na wanawake walikasirishwa na usalama duni na utendaji kazi wa hospitali hiyo.

Kwa upande wa Tanzania, sakata kama hili liliwahi tokea mwaka 2007.

Tarehe 8 Novemba, madaktari wawili wa upasuaji wa ubongo katika hospitali ya rufaa ya Muhimbili walimpasua kichwa Emmanuel Didas kutoa uvimbe ambao haukuwepo.

Wakati mgonjwa Emmanuel Mgaya, aliyekuwa na uvimbe huo alipasuliwa goti.

Madaktari hao walichukuliwa hatua na kufutwa kazi na mamlaka ya hospitali.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad