Msemaji wa Yanga Awapa Makavu Mashabiki wa Timu Hiyo "Acheni Kulaumu"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Msemaji wa Yanga Awapa Makavu Mashabiki wa Timu Hiyo "Acheni Kulaumu"
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wa mabingwa wa soka nchini Yanga SC, Dismas Ten amewaambia mashabiki wa timu hiyo kuacha kulaumu na kuwafundisha viongozi chakufanya bali waje uwanjani kuunga mkono timu zao.


Ten ameyasema hayo leo kwenye mkutano na wanahabari muda mchache kabla ya uzinduzi wa masuala ya kidijitali ya klabu hiyo, ambayo yatatoa huduma ya taarifa mbalimbali zinazohusu timu hiyo kwa mashabiki wake.

''Tunao mashabiki wengi kwasasa wamekuwa wakizungumza vitu vingi, kusema watu, kutukana watu ni wakati sasa wakuacha kufanya hivyo badala yake wajitokeze uwanjani kutoa nguvu ya 12 kusapoti wachezaji'', amesema Ten.



Ten pia amefafanua kuwa watu wengi walikuwa wanamuuliza kwanini hajaenda na timu Botswana ambapo amesema Yanga ni taasisi kubwa na ina wafanyakazi wengi ambao wanafanya majukumu wakati yeye yupo kwenye shughuli zingine za taasisi.

Ten amesisitiza kuwa masuala ya benchi la ufundi kupangiwa kikosi yameshapitwa na wakati, kwasababu benchi lina uwanja wake mpana wa kufanya maamuzi kwenye kikosi ili timu ifanye vizuri hivyo kila mtu afanye majukumu yanayomuhusu.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad