Rais wa TFF Afunguka Kuhusu Matumizi ya Mabilioni ya Fedha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Rais wa TFF Afunguka Kuhusu Matumizi ya Mabilioni ya Fedha
Rais wa Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF Wallace Karia leo amejitokeza mbele ya waandishi wa habari na kufafanua baadhi ya mambo yanayodaiwa kufanywa na TFF ikiwemo matumizi ya fedha kiasi cha bilioni 3.7.


Karia amesema fedha hizo zimetumika kwenye matumizi mbalimbali ya uendeshaji wa shughuli za mchezo wa soka nchini, ikiwemo Ligi mbalimbali nchini, vyama vya soka vya mikoa pamoja na malipo ya  wafanyakazi na mafunzo mbalimbali.

Aidha Rais Karia ameongeza kuwa ndani ya uongozi wake amefanikiwa kulipa deni la Bilioni 1.2 ambalo alilikuta TFF ikidaiwa na TRA, Mfuko wa Jamii (NSSF) pamoja na wafanyakazi na watoa huduma mbalimbali ndani ya shirikisho.



Kuhusu wafanyakazi kutopewa ajira Karia amesema ni kweli shirikisho limepunguza idadi ya wafanyakazi kutoka 44 mpaka 21, ambao wapo kwasasa huku wengine wakiwa wanajitolea na kufanya mafunzo kwa vitendo na endapo watafikia vigezo watapewa ajira za kudumu.

Moja ya mafanikio mengine ya uongozi wake Karia amesema ni kuingiza timu 4 za taifa za soka kambini kwaajili ya michuano mbalimbali ndani ya mwezi April. Timu hizo ni Taifa Stars, Twiga Stars, Ngorongoro Heroes na Serengeti Boys.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad