AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Simba ilitoka sare ya bao 3-3 na Stand katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa huku matokeo hayo yakiibakiza kileleni ikiwa na pointi 46 baada kucheza michezo 20 huku Yanga wakiwa nafasi ya pili na pointi 40 na ikiwa na mchezo mmoja mkononi kufuatia kucheza mechi 19.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara, alisema kuwa matokeo waliyopata katika mchezo dhidi ya Stand ni kama yamewatoa usingizini kwani wameshapanga mkakati mzito utakaoweza kuwapa ubingwa wa msimu huu.
“Kiukweli matokeo ya sare dhidi ya Stand kwanza hatukuyategemea kabisa lakini imetokea, mashabiki hawapaswi kulalamika na watambue haiwezekani kila siku tushinde sisi, ila kitu kizuri ni kwamba hatujafungwa, sasa hao wanaoshangilia sijui wanashangilia kitu gani.
“Stand wametuamsha sasa tunaelewa na tumeweka mkakaki mzito wa kuhakikisha tunachukua ubingwa wa msimu huu na hatutaki yajirudie ya msimu uliopita lakini hao wanaoshangilia sare yetu wakumbuke tuna mechi nao ambayo tutawafunga na kuweza kuchukua ubingwa wa msimu huu,” alisema Manara.
Simba na Yanga zinatarajiwa kukutana Aprili 7, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mchezo wa ligi kuu.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK