WCB Watoa Tamko Baada ya Diamond Kufungiwa Nyimbo Mbili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

WCB Watoa Tamko Baada ya Diamond Kufungiwa Nyimbo Mbili
Mara baada ya kufungiwa kwa ngoma mbili za Diamond ‘Waka na Hallelujah’, uongozi wa WCB umetoa tamko.

Meneja wa WCB, Sallam SK amesema kabla ya kutoa ngoma zao huwa zinakaguliwa na mlezi wao ambao ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda.

Ameendelea kwa kusema bado hawaelewi sababu ya kufungiwa kwa ngoma hizo, hivyo mlevi wao ataweza kuliongelea hilo zaidi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Sallam SK ameandika;

Tumepigiwa simu na vyombo vya habari kila sehemu kuulizwa juu ya nyimbo mbili za Diamond kufungiwa, nimeona tukiwa kama taasisi huwaga tunafanya vitu kwa kutokukurupuka sie kamaWCB Wasafi tulipoona taasisi yetu inakuwa kubwa tukaomba ulezi kwa Mhe. Paul Makonda ambae ni kiongozi wa serikali mwenye kupenda maendeleo ya vijana.

Kwa hiyo nyimbo zote za WCB kabla ya kutoka lazima mlezi wetu azipitie, kuna nyimbo nyingi ameshazizuia na zinazotoka basi ameridhia yeye binafsi zitoke, kwahiyo sioni sababu ya nyimbo ya Hallelujah na Waka kufungiwa kama inavyosemekana maana sisi hatujapata barua ya kuwa nyimbo hizo zimefungiwa na kwa sababu ipi.

Kama kweli zimefungiwa basi mlezi wetu ataweza kuongea mengi zaidi yangu mimi.

Wiki iliyopita Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) ilitangaza kufungia baadhi ya nyimbo zilizooneka kutokuwa na maadili, miongoni mwa ngoma hizo ni Hallelujah ambayo Diamond ameshirikiana na Morgan Heritage na ile ya Waka aliyoshirikiana na Rick Ross.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad