AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Muigizaji huyo ameeleza hayo kufuatia ushirikiano ulionyeshwa na waigizaji wenzake katika mazishi ya video vixen, Agness Gerald ‘Masogange’ ambaye alizikwa jana mkoani Mbeya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza ameandika;
“Tunaishi kwa kujifunza na mara nyingi mitazamo ya nje sio halisi, naomba nimpongeze IreneUwoya kwa kuwa rafiki mwema a special kipindi hiki, nimemuona akishiriki na kwenye utulivu sana yaani kasimama kama rafiki na hivi ndio inavyo takiwa, yaani jambo linapo kufika la mtu wa karibu sio kulia sana au kupoteza fahamu lazima usimame ujue hatma ya mwenzio kwanza,” amesema.
Aliendelea kwa kuwapongeza Zamaradi Mketema, Steve Nyerere, Aunty Ezekiel, Husna Maulid, Husna Sajent, Shilole kwa kusimamia vizuri tukio hilo vizuri.
“Nahisi Bongo Movie tuna vitu vikubwa sana wote kwa pamoja lakini sijui tunakosea wapi, maana kwa ushirikiano huo huo wa msibani, urudi kwenye kwenye kazi naamini kuna hatua kubwa sana tutapiga, nisema tu mpo vizuri sana, nyinyi ni wa maana sana,” ameongeza.
Hapo jana April 23, 2018 alizikwa Agness Gerald ‘Masogange’ ambaye alikuwa video vixen na muigizaji wa filamu, Masogange alifariki April 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar es Salaam.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK