Mbeya City Yakataa Kufungwa Kwao Yagawana Point na Yanga

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mbeya City Yakataa Kufungwa Kwao Yagawana Point na Yanga
Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara Yanga, wamebanwa mbavu ugenini na Mbeya City na kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Mchezo huo ambao uligubikwa na vurugu za hapa na pale ulishuhudia wageni Yanga, wakifunga bao la kuongoza dakika ya 57 kupitia kwa kiungo Raphael Daud ambaye amesajiliwa msimu huu kutoka Mbeya City.
Bao hilo lilisababisha vurugu za mashabiki lakini baadae walitulia na mchezo ukaendelea hadi dakika ya 67 ambapo mlinzi wa kati wa Mbeya City Ramadhan Malima kuoneshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Juma Abdul.
Mashabiki walianza kurusha mawe uwanjani na kupelekea Jeshi la polisi kutumia mabomu ya machozi kuweza kutuliza vurugu hizo na mchezo kuendelea. Mbeya City waliendelea kucheza pungufu.
Tukio la mvuto zaidi katika mchezo wa leo ni bao la kusawazisha la Mbeya City ambalo limefungwa dakika ya 90 na mshambuliaji ambaye aliingia akitokea benchi na kufunga bao hilo ambalo limeamua mchezo umalizike kwa sare.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad