Mrisho Gambo Awapa Somo Wanaume Wanaochepuka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mrisho Gambo Awapa Somo Wanaume Wanaochepuka
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amewataka wanaume wote wanaochepuka na kunyanyasa familia zao waache mara moja kitendo hicho kwani sio kitendo cha kiungwana kwa mwanaume anayejitambua.

RC Gambo amewashauri wanaume wote wenye tabia hizo kuacha mara moja na kama watashindwa basi ni bora wakafanya mambo yao kimya kimya na kuheshimu familia zao kwani vitendo hivyo husababisha magonjwa kwenye familia.

“Familia nyingi zipo kwenye mateso kutokana na matendo ya wanaume. Nadhani haya mambo ni sababu kubwa za Presha na sukari kwa familia nyingi. Wanaume ni busara kuheshimu nyumba yako hata kama una vituko vyako.“ameeleza RC Gambo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kusisitiza.

“Mwanamke mnaanza nae maisha, mnateseka nae mkiwa hamna chochote halafu Mungu anakupa riziki unaamua kumtesa mkeo. Wakati mwingine mwanaume unachukua hata chakula Cha ndani (unga , mchele, sukari na nk) alichokihangaikia mkeo kwa ajili ya watoto wake na kupeleka nyumba NDOGO.“ameandika Gambo.

Kwa upande mwingine Gambo amesema huu ni muda muafaka kuliangalia tatizo hilo kitaifa kwani familia nyingi zimekumbwa na janga hilo, “Kama Taifa tunahitaji tiba mbadala ya kuzisaidia familia zetu!“.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad