Serikali Haitamwonea Huruma Mtu Yoyote Awe Hapa au Nchi ya Nje- Rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Haitamwonea Huruma Mtu Yoyote Awe Hapa au Nchi ya Nje- Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema kwamba serikali zote mbili hazitamvumilia mtu yeyote ambaye ana lengo la kuuvunja Muungano.


Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akihutubia umma uliohudhuria kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwenye uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.
Rais Magufuli amesema kwamba Muungano ni mali ya Watanzania hivyo ni jukumu la kila mmoja kuulinda, kwani ndio silaha yetu kama nchi.

"Kwanza napenda kurudia kuwakumbusha Watanzania wenzangu kwamba Muungano wetu ndiyo nguvu yetu na ndio silaha yetu, kila mmoja ana wajibu wa kuulinda. Serikali zote mbili za Tanzania Bara na Zanzibar, kamwe hatutamwonea huruma mtu yeyote, awe raia wa hapa nchini au wa nje ya nchi, atakayetaka kuvunja muungano wetu”, amesema Rais Magufuli.

Pia Ras Magufuli amesema kwamba kufikisha miaka 54 ya Muungano sio kitu rahisi na pia ni kitu cha kujivunia, kwani wapo ambao walijaribu kuungana lakini wameshindwa kudumu kwenye muungano huo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad