Uda-rt Yafunga Barabara ya Jangwani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Uda-rt Yafunga Barabara ya Jangwani
Kampuni inayotoa huduma katika mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (Uda-rt), imelazimika kusitisha huduma kwa baadhi ya njia.

Taarifa ya Uda-rt imesema huduma za mabasi hayo kwa baadhi ya njia zimesitishwa kuanzia saa 11:00 alfajiri leo Jumatatu Aprili 16, 2018 kutokana na kufungwa Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani.

Barabara hiyo imefungwa kwa sababu ya mafuriko yaliyosababisha maji kupita juu ya daraja la Mto Msimbazi.

“Kwa sasa huduma zinatolewa kwa njia za Mbezi – Kimara; Kimara – Morocco; Kimara - Magomeni Mapipa; Kivukoni – Muhimbili; Gerezani – Kivukoni; na Gerezani – Muhimbili,” inasema taarifa ya Uda-rt iliyotolewa na mkuu wa kitengo cha mawasiliano, Deus Bugaywa.

Kampuni hiyo inasema huduma kamili zitarejea baada ya barabara kufunguliwa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad