Serikali Yatangaza Vita na Wanaowapeleka Wasichana Nje Kufanya Biashara ya Ngono

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali Yatangaza Vita na Wanaowapeleka Wasichana Nje Kufanya Biashara ya Ngono
Serikali imesema wajibu wake kuhakikisha Watanzania wanaopata fursa ya kufanya kazi nje ya mipaka ya Tanzania wanafanya kazi katika Mazingira mazuri na yanayolinda staha na utu wao.

Serikali imesema kama kuna wasichana wanapelekwa nje ya nchi yakufanya biashara ya ngono ikijulikana haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya wanaofanya hivyo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba ametoa ufafanuzi huo, leo Mei 21 Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge, Hawa Mchafu aliyeuliza,

Je ni hatua gani kali zinazochukuliwa dhidi ya wafanya biashara wanaosafirisha vijana wa Kitanzania hususani vijana wa kike kwenda nje ya nchi kwaajili ya kufanya biashara isiyo rasmi ikiwemo kuuza miili yao.? Ni ipi sasa kauli ya serikali dhidi ya madai ya kusikitisha sana kuwa baadhi ya Watanzania wanasafirishwa kwenda nje wanaenda kuuzwa figo zao?

“Kuhusu hatua gani kali zimechukuliwa kuhusu wafanya biashara ambao wamewapeleka wasichana nje kwenda kufanya biashara ya kuuza miili yao kwa kweli niseme kwamba hiyo ikijulikana hatua kali za nchi yetu zitachukuliwa lakini so far mimi sina data za aina hiyo,” amesema Dkt. Kolimba.

“Lakini kuhusu kwamba kuna Watanzania ambao wamepelekwa nje na kwamba wanapopelekwa nje figo zinachukuliwa hilo pia sisi tutafuatilia kama kuna ukweli hatua kali zitachukuliwa kwenye nchi husika.”
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad