AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mara baada ya kuibuka mjadala uliozua gumzo mitandaoni kuhusiana na shambulio la aibu dhidi ya wanawake eatv.tv ilimtafuta mwanasheria ili kupata ufafanuzi kuhusu shambulio hilo ambapo, Wakili wakujitegemea Johanes Konda amesema kwamba wanawake wengi hawatambui kama kukonyezwa bila ridhaa yao ni kosa kisheria.
"Kanuni za adhabu sura ya 16 ndio inaelezea zaidi kuhusiana na shambulio la aibu lakini kulingana na mazingira na tamaduni zilizopo sasa, dada zetu wanaona kawaida tuu lakini sheria imewekwa kwa ajili ya kuwatetea wao dhidi ya shambulio hilo ambalo linaweza kuwa ni kwa kuguswa au kwa ishara kama kukonyeza au kupiga kelele za kuashiria kuna kitu cha tofauti kimepita", amesema Wakili Konda.
Wakili Konda amesema kuwa endapo wahusika ambao ni wanawake wakizitambua haki zao na kuwashitaki watuhumiwa wanaweza kusaidia kuondoa tabia hizo na endapo ikithibitika basi adhabu yake ni kuanzia miaka isiyozidi 10 kushuka chini.
Hivi karibuni Kamanda wa Polisi wa mkoa wa mjini Magharibi Kamishna Msaidizi Mwandamizi Hassan Nassir amesema ni marufuku kukohoa pale unapopishana au unapomwona mwanamke mwenye makalio makubwa kwamba kukohoa huko kutapelekea kukamatwa kwa maana kitendo hicho ni 'shambulio la aibu”.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK