Bocco atwaa Tuzo ya Mchezaji bora wa Ligi kuu bara

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mshambuliaji wa klabu ya Simba, John Bocco, ameibuka mshindi wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2017/18.

Bocco ametwaa tuzo hiyo huku akiwapiku wachezaji wenzake beki Erasto Nyoni na Emmanuel Okwi ambao pia walikuwa kwenye kinyang'anyiro.

Ukiachana na tuzo ya mchezaji bora VPL, Bocco ambaye ni Nahodha wa kikosi cha Simba amekuwa na msimu mzuri kwa kufanikiwa kubeba pia tuzo ya Mo akiwa mchezaji bora ndani ya timu hiyo.

Vodacom ambao ni wadhamini wakuu wa ligi wamempatia kitita sha shilingi milioni 12 Bocco kama zawadi kutokana na kitengo cha kinyang'anyiro alichokuwa amewekwa.

Okwi ambaye ameshindwa katika kitengo hicho, ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kwa kufikisha idadi ya mabao 17 aliyofunga sambamba na zawadi ya shilingi milioni 3.

Aidha, timu bingwa ambayo ni Simba imepokea kitita cha fedha, shilingi milioni 96 huku Azam ambao ni washindi wa pili wakibeba milioni 48 na Yanga waliomaliza msimu wakiwa namba 3 wakijinyakulia milioni 27.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad