AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Juni 12, 2018 wakati alipokuwa anafanya ukaguzi wa Msikiti Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) unaojengwa Kinondoni Jijini Dar es Salaam kwa kupitia mfadhili Mfalme Mohammed wa sita kutoka Morocco.
"Mkishakuwa na wasemaji wengi katika masuala ya dini hata yale mnayoyasema yanakosa maana na mara nyingi huwa yanakosa muelekeo na wasikilizaji hawataelewa kuwa hayo yanayosemwa yanatoka kwa viongozi wa dini au na wengine waliotumwa na wanaotumwa mara nyingi wanapenda kuweka chumvi kwa manufaa yao binafsi", amesema Rais Magufuli.
Pamoja na hayo, Magufuli ameendelea kwa kusema "panapozungumzwa neno lolote linalohusu masuala ya dini au ushauri wowote unaohusika na dini, unapaswa uzungumzwe na watu wa dini wenyewe kama ni masheikh azungumze Mufti, kama Mchungaji azungumze Mchungaji msitafute wasemaji kwa niaba yenu, mtakuwa mnatupoteza pabaya".
Mbali na hilo, Rais Magufuli amewahakikisha viongozi wa dini zote nchini kuendelea kushirikiana nao kwa hali na mali kwa kuwa serikali haina dini.
"Napenda kuwaahidi viongozi wa dini zote kwamba serikali yangu itaendelea kushirikiana na dini zote na niendelee kuwaomba viongozi wa dini msiwe na wasemaji ambao sio viongozi wa dini. Mnapokuwa viongozi wa dini halafu mkawatumia wasemaji ambao sio viongozi wa dini labda ni wanasiasa, mtakuwa mnachanganya dini na siasa ambacho ni kitu kibaya sana", amesisitiza Magufuli.
Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amepewa ahadi na wakandarasi wa ujenzi wa msikiti huo ambao utakuwa unabeba zaidi ya watu elfu nane (8,000) kuwa unatarajiwa kukamilika mwaka 2019 kati ya mwezi Aprili au Mei
Chanzo: EATV
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK