AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Wilfred Dyansobera, Ijumaa iliyopita kufuatia maombi yaliyowasilishwa na Bodi ya Wadhamini wa chama hicho, kambi ya Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.
Bodi hiyo kupitia kwa mawakili wake Juma Nassoro na Daimu Halfani waliwasilisha mahakamani hapo maombi hayo, baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuruhusu ruzuku ya zaidi ya Sh.600 milioni.
Msajili wa Vyama alitoa kiasi hicho cha ruzuku kwa chama hicho, kambi ya Mwenyekiti wake wa Taifa anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba, licha ya kuwepo kwa amri ya kumzuia kutoa ruzuku kwa chama hicho kambi yoyote.
Kufuatia maombi hayo, Jaji Dyansobera katika uamuzi wake wa Ijumaa ametoa amri ya kuzizuia benki zote nchini kutoa ruzuku ya Serikali kwa chama hicho kambi yoyote kulingana na uamuzi wake wa awali dhidi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Kwa uamuzi huu chama hicho hakitaweza kutoa pesa yoyote katika akaunti zake zinazohusiana na ruzuku ya Serikali, hadi kesi zilizoko mahakamani zinazotokana na mgogoro huo wa uongozi zitakapoamuriwa.
Chanzo: Mwananchi
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK