Mambosasa Awatangazia Kiama Matapeli kwa Njia ya Mitandao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mambosasa Awatangazia Kiama Matapeli kwa Njia ya Mitandao
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa Jeshi la Polisi kushirikiana na TCRA kuna watu wanaotapeli kwa njia ya mtandao wameshawakamata na jambo hilo bado linafanyiwa kazi.



Akizungumza na Redio Times Fm, leo Juni 13, 2018 amesema kuwa jeshi lake litahakikisha linafanya juhudi wananchi hawatapeliwi.

“Utapeli ambao umekithiri ni wa kimtandao, mtu unatumiwa meseji kwamba umeshinda kiasi fulani kwa hivyo unatakiwa kutuma kiasi fulani ili upatiwe kiasi hicho, Wananchi wengi wamelizwa na utapeli huo lakini Polisi sasa hivi tunafanyia kazi,” amesema Kamanda Mambosasa.

“Sisi tuna ushirikiano wa karibu sana na TCRA na mpaka sasa kuna baadhi ya watu wanaotapeli wananchi kwa njia ya mtandao tumeshawakamata na bado tunaendelea na juhudi za kuhakikisha wananchi hawatapeliwi,” ameongeza Mambosasa.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad