AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Shirika la habari la Reuters lilinukuu chanzo kimoja kikisema kuwa Kim anatarajiwa kusafiri hadi katika uwanja wa ndege wa Changi, Singapore leo Jumapili.
Juhudi za Reuters kutaka kupata uhakika kutoka mamlaka za usafiri wa anga Singapore ziligonga mwamba baada ya kukataa kuzumgumzia safari hiyo ya Kim.
Kim na Trump pamoja na mambo mengine watajadili ajenda ya kuondoa silaha za nyuklia katika Rasi ya Korea na kwamba rais huyo wa Marekani anatarajiwa kumtaka Kim kuachana na uundaji wa silaha hizo.
Wakati Kim akijiandaa kuwasili leo kwa ajili ya mkutano huo wa kihistoria, viongozi wakuu wa nchi zilizoendelea zaidi kiviwanda duniani (G7) Ijumaa walianza mkutano wa siku mbili nchini Canada ambao mada kuu ni biashara duniani na Korea Kaskazini.
Mkutano huo ulifanyika Charlevoix katika jimbo la Quebec lililopo mashariki mwa Canada.
Biashara huru na uchumi wa dunia ilikuwa mada kuu katika siku ya kwanza. Mkutano huo unafuatia hatua ya Rais Donald Trump kuendelea na msimamo wake wa kulinda masoko ya ndani,ushuru wa forodha katika bidhaa za chuma cha pua na alumini uliowekwa na utawala wa Trump umeifanya Marekani kutofautiana na mataifa mengine ya G7.
Katika kikao cha jana Ijumaa, vyanzo vya habari vilisema kuwa Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe aliwaambia viongozi wenzake kuwa majibizano ya vikwazo vya kibiashara ya papo kwa papo yataathiri uchumi wa dunia kwa kiwango kikubwa na hayatamnufaisha mtu yeyote.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK