Trump Ataka Wahamiaji Haramu Watimuliwe Haraka Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Trump Ataka Wahamiaji Haramu Watimuliwe Haraka Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito wa kuharakishwa kwa shughuli ya kuwatimua wahamiaji haramu nchini humo bila hata kufuata utaratibu wa mahakama.

Amefanya hivyo kupitia msururu wa ujumbe kwenye Twitter.

"Mtu anapoingia ndani, ni lazima mara moja, bila majaji na kesi mahakamani, tuwarejeshe walikotoka," Trump ameandika.

Amesema hayo siku chache baada yake kubatilisha sera ya kuwatenganisha watoto wa wahamiaji na wazazi wao baada ya sera hiyo kushutumiwa vikali Marekani na nje ya nchi hiyo.

Takwimu zinaonesha watoto 2,300 walikuwa wametenganishwa na wazazi wao kati ya Mei na Juni mwaka huu.

Kuanzia mwezi Mei, wahamiaji wanaovuka mpaka wa Marekani na kuingia nchini humo kinyume cha sheria wanakabiliwa na hatari ya kufunguliwa mashtaka ya jinai chini ya sera ya Trump ya kutowavumilia wahamiaji.

Rais Trump hajatofautisha kati ya wahamiaji wa kiuchumi na wale wanaotafuta hifadhi kutokana na mateso na kudhalilishwa mataifa yao.

Rais huyo amekuwa akishutumiwa hata na viongozi wa chama chake cha Republican kwa lugha kali aliyoitumia kwenye Twitter.

Aliposema awali kwamba wahamiaji wanatishia "kufurika na kuiambukiza nchi yetu, mbunge mwanamke wa chama cha Republican Ileana Ros-Lehtinen alimjibu kwenye Twitter akisema tamko lake halina msingi, "linakera" na linadunisha wale wanaotafuta maisha mazuri.

Maafisa wa uhamiaji Marekani wanasema watoto 2,342 walitenganishwa na wazazi 2,206 kati ya 5 Mei na 9 Juni.

Mnamo 20 Juni, Trump aililegeza msimamo wake wa kuunga mkono sera hiyo kali na badala yake akatia saini agizo la rais la kusitisha hatua hiyo ya kuzitenganisha familia.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad