CHADEMA yapata kigugumizi kuhusu Madiwani wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

CHADEMA yapata kigugumizi kuhusu Madiwani wake
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepatwa na kigugumizi kutaja sababu ya kuwavua uanachama madiwani wake watatu siku ya jana (Jumamosi, Julai 22) na kubaki wakisisitiza ni utovu wa nidhamu.


Akizungumza na www.eatv.tv, Mkurugenzi wa Itifaki na Mawasiliano ya Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema amewataja madiwani waliovuliwa uanachama kuwa ni Geofrey Kajigili wa Kata ya Sisimba, Newton Mwatujobe wa Kata ya Manga na Humphrey Ngalawa wa kata ya Iwambi Jijini Mbeya huku akishindwa kutaja sababu iliyopelekea maamuzi hayo kufanyika kwa kudai suala hilo lipo kwenye uchunguzi.

 "Ni kweli tumewavua uanachama Madiwani hao watatu kutokana na vitendo vyao vya utovu wa nidhamu walivyovionyesha ambavyo vinakinzana na chama chetu. Siwezi kusema nini hasa wamekifanya kwa kuwa jambo hilo kwa  sasa lipo kwenye Kamati Kuu linasubiriwa kufanyiwa maamuzi", amesema Mrema.

 Pamoja na hayo, Mrema amesema kwa sasa hawezi thibitisha jambo lolote kuhusu diwani Kajigili kudaiwa kumpigia kampeni hadharani Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson, kwamba anastahili kuwa Mbunge wa Mbeya mjini mpaka pale Kamati Kuu itakapotoa maamuzi yao juu ya uchunguzi ambao wanaufanya.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad