AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mfanyabiashara huyo anayemiliki kampuni ya mabasi ya Zakaria yanayosafiri kati ya mikoa ya Mwanza, Simiyu na Mara alifikishwa mahakamani Julai 5 akikabiliwa na mashtaka mawili ya kujaribu kuua kwa kutumia silaha baada kwa kuwajeruhi kwa risasi Ahmed Segule na Issac Bwire.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Rahimu Mushi, wakili wa Jamhuri, Lukelo Samuel aliiomba Mahakama kuzuia dhamana ya mshtakiwa akidai hali za majeruhi wa tukio hilo lililotokea Juni 29 si nzuri na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu.
Mawakili wa utetezi Kassim Gila na Onyango Otieno walipinga ombi hilo wakisema hakuna nyaraka wala uthibitisho uliowasilishwa mahakamani kuthibitisha kuwa hali za majeruhi ni mbaya na wamelazwa hospitalini.
Baada ya kusikiliza hoja za zote mbili, Hakimu Mushi aliahirisha shauri hilo hadi leo Julai 10 ambapo anatarajiiwa kutoa uamuzi wa kuhusu dhamana.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK