AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kauli hiyo, aliitoa juzi jioni baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Boko Beach Veterani jijini Dar es Salaam.
Simba tayari imefanikiwa kuwasajili wachezaji sita hadi sasa ambao ni Adam Salamba, Mohammed Rashid, Meddie Kagere, Abdul Mohammed, Marcel Boniventure na Pascal Wawa.
Akizungumza na Championi Jumatano, Djuma alisema katika usajili huo wa wachezaji 30, wanataka kubakisha nafasi tatu pekee kwa ajili ya kuongeza katika usajili wa dirisha dogo kama akihitajika mchezaji kwa ajili ya kukiimarisha kikosi chao.
Djuma alisema, wachezaji watakaobaki kuichezea Simba ni wale watakaoweza kupambana ndani ya uwanja katika kuipa matokeo mazuri huku akiahidi kuwaondoa baadhi ya wachezaji wenye mikataba kwenda kwenye klabu nyingine kwa ajili ya kulinda viwango vyao.
“Sidhani kama ni sawa kuendelea kukaa na mchezaji mwenye mkataba kwenye timu wakati hana nafasi ya kucheza katika kikosi changu, hivyo nimeona ni vema nikamuachia kwenda kwa mkopo kwingine kwa ajili ya kwenda kucheza kuliko aendelee kukaa benchi.
“Hivyo, hiyo inaweza kumsababishia mchezaji kuua kiwango chake kama mfano kipa wetu Mseja msimu uliopita wa ligi hakupata nafasi ya kucheza, hivyo kama kocha nimeshauri tumtoe kwa mkopo ili aende kwingine akacheze.
“Na hilo tayari nimelifanyia kazi na kuutarifu uongozi, hivyo Mseja hatakuwa katika sehemu ya kikosi chetu, pia wapo wengine ambao hivi karibuni nitawaweka wazi,” alisema Djuma.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK