AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amekanusha taarifa za chama hicho kumpa barua ya onyo mbunge wa Mtama, Nape Nnauye.
Akizungumza leo Alhamisi Julai 5, 2018 Polepole amesema mbunge huyo wa CCM hajapewa barua ya onyo, kwamba chama hicho tawala kina taratibu zake.
Taarifa za Nape kupewa barua hiyo zimesambaa mitandaoni huku mwenyewe akikanusha kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter.
Taarifa hizo zilitiwa chumvi zaidi baada ya kuhusishwa na msimamo wa Nape katika suala la Korosho lililoibuka katika Bunge la Bajeti.
Katika mkutano huo wa Bunge, Nape na wabunge wenzake kutoka mikoa ya Kusini walipinga uamuzi wa Serikali wa kubadilisha Sheria ya Korosho, ikiwa ni pamoja na fedha za ushuru wa korosho kwenda katika mfuko mkuu wa Hazina.
Akizungumza baada ya uwasilishwaji wa ripoti ya taasisi ya Twaweza jijini Dar es Salaam, Polepole amesema chama hicho tawala kina utaratibu wa vikao linapotokea tatizo la mwanachama wake.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK