AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ameonya pia kwamba iwapo mfungwa atakamatwa na simu gerezani, mkuu wa gereza husika atakuwa amepoteza sifa za kazi yake.
Lugola ameyasema hayo leo alipozungumza na vyombo vya habari na kusisitiza wito wa Rais John Magufuli wa kutaka wafungwa wajitegemee kwa chakula na kuhakikisha wafungwa hawaingizi simu gerezani.
“Nimemuelekeza Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini kutengeneza mkakati maalum kuhakikisha wafungwa wote nchini wanajilisha kuanzia mboga, kama ni kufuga samaki au kulima maharage, na kusiwe na kisingizio chochote kwani jambo hili linatekelezeka,” alisema.
Alisema bunge lijalo litaanza kubadilisha sheria ili kusiwe na kinga kwa wafungwa ili wafanye kazi, wajilishe na wawalishe mahabusu, na ikiwezekana magereza yazalishe chakula cha ziada kwa kuuza na kutengeneza kipato.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK