Hizi Hapa Sababu za Trump Kujenga Kikosi Kipya cha Jeshi la Anga za Mbali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wana anga hawatapewa silaha hivi karibuni lakini kulingana na makamu wa rais wa Marekani Mike Pence, ni kuwa China na Urusi wamekuwa wakiunda silaha za kushambulia setilaiti ambazo pia zinatakiwa kukabiliwa.

Kenya yatengeneza setilaiti yake ya kwanza
"Mazingira ya anga za mbali yamebadilika miaka iliyopita," alisema Pence wakati alikuwa akieleza kile kikosi hicho kipya kitafanya.

Alisema kutabuniwa kikosi cha jeshi ambacho kitakuwa na majukumu ya kulinda maslahi ya Marekani kama vile setilaiti zinazotumiwa kwa mawasiano na ujasusi.

The space shuttle Discovery made its final mission to the International Space Station in 2011
Rais Trump ambaye aliuzungumzia mpango huo mapema mwaka huu alionya kuhusu hatua hizo za kijeshi zimechukuliwa na washindani wa Marekani.

Rais Alisema: "Nimeona vitu ambavyo hamngetaka hata kuviona."

Kuna huduma za kijeshi na za kiraia kwenye anga za mbali lakini wakati mwingine zinaweza kukutana.

Kijana aliyeunda setilaiti ndogo zaidi India
Teknolojia ya mawasialio ya setilaiti inayofahamika kama Global Positioning System (GPS) ilianzishwa na jeshi la Marekani lakini baadaye iliruhusiwa kwa matumizi ya kiraia.

Anga za mbali zimekuwa zikitumiwa kwa masuala ya kijeshi tangu miaka ya sitini, anasema Alexandria Stickings

Wakati wa vita baridi Marekani na muungano wa usovieti hakuwa na vita kwenye anga za mbali lakini walitumia setilaiti kuchunguzana.

India yaweka rekodi ya kurusha satelaiti
China, Urusi na Marekani wamefanyia majaribio salaha ambazo zina uwezo wa kuharibu setilaiti.

Haya ni makombora yanayoweza kurushwa kutoka duniani moja kwa moja kwenda kuigonga setilaiti kenye orbit.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad