Huu ndio Mkoa Unaongoza Kwa Udhalilishaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Jamii imetakiwa  irudi katika  dini zao pamoja na kurudisha malezi ya zamani kwa lengo la kupunguza au kuondoa kabisa  vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.

Hayo yameelezwa na mkuu wa dawati la jinsia na watoto mkoa wa kusini Ali Mohammed Othmani  wakati akitoa elimu juu ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanafunzi wazazi,walezi pamoja na walimu huko makunduchi mkoa wa kusini unguja. 

Amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa  mkoa wa kusini unaongoza kwa kesi za udhalillishaji  ikiwemo kubaka,kulawiti  na mengineyo  jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya wanafunzi  na kushuka kwa kiwango cha elimu  pamoja na kushuka nguvu kazi ya taifa. 

Nae afisa wa  dawati la jinsia na watoto shuwekh Zuberi amefafanua madhara  ya ukatili ambayo yanaweza kumpata  muathirika wa tatizo hilo ni pamoja na kuathirika kisaikolojia, kupata ulemavu na hata kupata maumivu makali  katika mwili wake. 

Kwa upande wake diwani wa wadi ya makunduchi Zawadi Hamdu amewashukuru dawati la jinsia kwa kuja kutoa elimu na amewataka  wawe mstari wa mbele katika kushulikia kesi zao ili kuweza kupatiwa hukumu mapema.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad