Kamati Ya Bunge Yaitaka Serikali Kukutana Na Wenye Viwanda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kamati Ya Bunge Yaitaka Serikali Kukutana Na Wenye Viwanda
Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imeitaka serikali kukaa na wamiliki wa viwanda nchini na kuhakiki gharama za uzalishaji ambazo zimekuwa zikisababisha bidhaa za wazalishaji wa ndani kushindwa kushindana na zinazoingizwa nchini.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Sadick Murad ametoa kauli hiyo  jana Agosti 13, wakati kamati hiyo ilipotembelea kiwanda cha uzalishaji wa mabati na vifaa vingine Alaf.

Murad amesema gharama za uzalisha zimekuwa kikwazo kwa viwanda vya ndani ambazo vinazalisha bidhaa kwa bei ghali ilihali zinazoingizwa nchini zinauzwa kwa bei rahisi.

“Gharama za uzalisha zikiwa fair na wazalishaji wa ndani kupunguziwa kodi za umeme na tozo nyingine, gharama za uzalishaji zitashuka,” amesema ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero (CCM).

Aidha, alitoa wito kwa wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji, kuisimamia vema Shirika la Viwango (TBS) na Mamlaka ya Mapato (TRA) ili ziendelee kutoa huduma rafiki kwa wazalishaji wa ndani ambao wamekuwa chachu katika uzalishaji wa ajira na ukuzajia uchumi.

Hata hivyo, Katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Joseph Buchweshaija amesema tayari imeandaa mpango maalumu wa kwa kushirikiana na TBS kuondoa bidhaa hafifu sokoni. Tayari tumeanza kuisafisha suala hilo na ninawaahidi kuendelea kutekeleza yote mliyoagiza,” amesema.

Aidha,  Meneja Mkuu wa kiwanda hicho cha Alaf, Dipti Mohanty aliieleza kamati hiyo kuwa umeme umeendelea kuwa mojawapo ya kikwazo kikubwa katika uzalishaji wa bidhaa zao.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad