Kiongozi wa Upinzani nchini ZimbabweTendai Biti Akamatwa Mpaka wa Zambia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kiongozi wa upinzani akamatwa Zimbabwe
Kiongozi wa juu wa upinzani nchini Zimbabwe Tendai Biti amekamatwa Jumatano wiki hii katika mpaka wa Zambia wakati ambapo chama chake kinaendelea kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais, amebaini mwanasheria wake.

Tume ya Uchaguzi nchini Zimbabwe (ZEC) ilimtangaza Emmerson Mnangagwa, kuwa alishinda uchaguzi huo kwa asilimia 50.8.

"Amekamatwa kwenye mpaka wa Zambia," Nqobizitha Millo amesema, akiongeza kwenye ujumbe wa simu (SMS) kwamba waziri huyo wa zamani alikuwa akitafuta "hifadhi" ya ukimbizi katika nchi jirani ya Zambia.

Mmoja kati ya viongozi wa juu wa upinzani, na waziri wa zamani wa Fedha wa Serikali ya Umoja wa kitaifa (mnamo mwaka 2009-2013), Biti anatafutwa na mahakamani, wbaada ya kushtumiwa kuchochea vurugu, kwa mujibu wa gazeti la The Chronicle, linalounga mkono serikali.

Bw Biti alitangaza kabla ya kutangazwa rasmi matokeo ya uchaguzi na Tume ya Uchaguzi kwamba Nelson Chamisa, mgombea wa chama chake cha Movement for Democratic Change (MDC) alishinda uchaguzi, huku akiishtumu Tume ya Uchaguzi kwa kutangaza matokeo tofauti.

Tume ya uchaguzi ilimtangaza Bw Mnangagwa, aliyekuwa mshirika wa karibu wa Robert Mugabe, aliyetimuliwa madarakani na jeshi mnamo mwezi Novemba baada ya miaka 37 ya kuitawala nchi hiyo, mshindi wa uchaguzi huo kwa asilimia 50.8.

Hatua ya vikosi vya usalama na ulinzi kuvunja maandamano ya upinzani ilisababisha watu sita kupoteza maisha.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad