Mashabiki wa Simba Wanusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali Wakielekea Mwanza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mashabiki wa Simba Wanusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali Wakielekea Mwanza
Gari iliyokuwa imewabeba mashabiki wa Simba tawi la Ubungo Terminal limepata ajali baada ya kumgonga mwanamke mmoja mwendesha baiskeli kisha kuacha njia maeneo ya Nzega Ndogo.



Mashabiki hao walikuwa wakielekea jijini Mwanza kushuhudia mchezo wa ngao ya jamii baina ya Simba dhidi ya Mtibwa Sugar.



Mwanamke huyo amepata majeraha na kukimbizwa hospitali wakati hakuna abiria aliyejeruhiwa ndani ya gari hilo licha ya kushindwa kuendelea na safari.

Mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba wanatarajia kushuka uwanja wa CCM Kirumba hii leo kuwakabili mabingwa wa FA klabu ya Mtibwa kwenye mchezo wa Ngao ya jamii ikiwa ni ishara ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad