Serena Williams Apigwa Stop Kuvaa Nguo Nyeusi French Open

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 Serena Williams Apigwa Stop Kuvaa Nguo Nyeusi  French Open
Mcheza tenisi maarufu duniani kwa upande wa wanawake, Serena Williams huenda akazuiwa kuvaa mavazi ya kubana yenye rangi nyeusi katika mchezo huo, kuelekea mashindano ya mwaka ujao ya French Open.


Hatua hiyo imekuja baada ya waandaaji wa mashindano hayo kuanzisha mchakato wa kuunda sheria mpya juu ya mavazi yanayohitajika katika mchezo huo.

Akizungumzia juu ya utaratibu huo mpya utakaoanzishwa, Rais wa shirikisho la tenisi nchini Ufaransa, Bernad Giudicelli amesema "mavazi hayo hayatokubalika tena, ninaamini kuna kitu ambacho sisi tumekwenda mbali sana, unatakiwa kuheshimu mchezo na mahali husika".

Japokuwa Rais huyo hakutaja hasa jinsi gani sheria hiyo itakavyokuwa lakini amesema wana mpango wa kulingana na sheria za mavazi za mashindano ya Wimbledon, ambayo wachezaji wote hulazimika kuvaa mavazi yenye rangi nyeupe pekee.

Kwa upande wake Serena Williams amesema kuwa, mavazi hayo yanamsaidia kuendana na tatizo lake la kuganda kwa damu, tatizo ambalo lilinusurika kumgharimu maisha yake wakati wa kujifungua.

Bingwa huyo mara 23 wa Grand Slam alirejea katika kinyang'anyiro hicho  kwenye michuano ya French Open mwezi Mei, kufuatia kumalizika kwa likizo yake baada ya kujifungua mtoto wa kike mwezi Septemba mwaka 2017.

Serena anatarajia kuusaka ubingwa wa saba wa taji la michuano ya US Open itakayoanza Jumatatu ya wiki ijayo, atakapopambana na mwanadada raia wa Poland, Magda Linette anayekamata nafasi ya 60 katika viwango vya tenisi duniani kwa sasa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad