Watu 82 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Indonesia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu 82 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Indonesia
Mamlaka nchini Indonesia inasema zaidi ya watu 82 wamefariki baada ya tetemeko kubwa la ardhi kukipiga kisiwa cha Lombok.

Maafisa wa idara ya kudhibiti majanga wanasema mamia ya watu wamejeruhiwa vibaya kwa tukio hilo lililotokea Jumapili.

Tetemeko hilo lenye nguvu ya 7 kwenye vipimo vya Richter limeharibu vibaya miundombinu ya umeme na barabara sambamba na nyumba.

Image caption
Tetemeko hili lilisababisha watu kuchanganyikiwa
Katika kisiwa jirani cha Bali picha za video zimeonyesha watu wakikimbia majumbani mwao huku wakipiga kelele za msaada.

Tetemeko hili limekuja wiki moja baada ya jingingine kuipiga sehemu hiyo ya Lombok, kisiwa maarufu kwa shughuli za utalii ambapo watu 16 waliuawa.

Nyani albino aokolewa nchini Indonesia
Mvulana amuoa ajuza wa miaka 70
Hatari ya kuwepo kwa kwa kimbunga ilitangazwa kisiwani hapo lakini ikaondolewa saa chache baadae.

Msemaji wa idara ya kudhibiti majanga ya Indonesia amesema nyumba nyingi zimeathirika vibaya, ambapo nyingi kati ya hizo zilijengwa kwa kutumia nyenzo duni.

Waziri wa mambo ya ndani wa Singapore Kasiviswanathan Shanmugam alikua ziarani katika kisiwa hicho ambapo ametuma picha kwenye mitandao ya kijamii akionyesha namna chumba chake kilivyoathirika.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad