Meli mbili za Mv Nyakibare na Orion II, Zawasili Ukara Kukinusuru Kivuko cha Mv Nyerere

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Meli mbili za Mv Nyakibare na Orion II, Zawasili Ukara Kukinusuru Kivuko cha Mv Nyerere
Mitambo na vifaa maalum vya kunyanyua, kubeba na kuvuta vitu vizito imewasili katika gati ya Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe tayari kufanya kazi ya kunyanyua na kugeuza kivuko cha Mv Nyerere kilichopinduka katika ziwa Victoria.

Mpaka kufikia jana wataalam wa uokoaji na masuala ya majini walifanikiwa kukilaza ubavu kivuko hicho ambacho awali kililala kifudifudi tangu kilipopinduka Septemba 20.

Mitambo na vifaa hivyo vimewasili asubuhi ya leo vikiwa ndani ya meli mbili kubwa binafsi za Mv Nyakibaria ya kampuni ya Mkombozi and Fisheries na Mv Orion II inayomilikiwa na kampuni ya Kamanga Ferry, zote za jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jioni, Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa ya Mv Nyerere, Isaac Kamwelwe alisema mitambo na vifaa hivyo vitarahisisha kazi ya kunyanyua, kugeuza na kukivutia ufukweni kivuko hicho.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad