AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna, amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Kennedy Obworo, mwenye umri wa miaka 35, ambaye amekuwa akiwawekea wanawake dawa za kulevya katika vinywaji na kisha kuwabaka na kuwaibia vitu walivyonavyo.
Katika tukio jingine, jeshi hilo linamshikilia Sheshe Mazoya, anayedaiwa kuwa mganga wa kienyeji mkazi wa Wilaya ya Magu kwa kosa la kukutwa na nyara mbalimbali za serikali ikiwemo mikia miwili ya nyumbu na pembe moja ya swala, kucha za Simba na miiba ya nungunungu ambavyo alikuwa anavimiliki kinyume na sheria.
Aidha, Kamanda Shanna amesema wanamshikilia mwanamke anayefahamika kwa jina la Sonia Fanuel kwa kosa la wizi wa kufungua milango kwa kutumia funguo bandia.
Kamanda Shanna ambaye amechukua nafasi ya Kamanda Ahmed Msangi aliyehamishiwa makao makuu, amesema watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani Jumatatu ijayo kujibu tuhuma zinazowakabili.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK