Steve Awaomba Wasanii Wote Wasimame na Wasanii Wenzao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa Bongo movie na komedian maarufu Steve Nyerere ameibuka na kuwataka Wasanii Wenzake wote kuungana pamoja na kuwaombea msamaha wasanii wenzao.

Steve amewataka wasanii wote kwa jumla bila kujali wa muziki au filamu kuwa pamoja kumuombea msamaha msanii wa Bongo Fleva, Maua Sama ambaye mpaka sasa yupo kituoni kwa kosa la uharibifu wa mali ya umma.

Maua na mtangazaji wa Clouds, Soudy Brown wanadaiwa kusambaza video mitandaoni ikionesha watu wanaokanyaga noti za shilingi elfu kumi ambalo ni kosa la kisheria.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers,  Steve Nyerere amesema  anawaomba wasanii waungane kumuombea msamaha Maua kwani ni mwenzao.

Msanii yeyote ni kioo cha jamii, chochote atakachokifanya kinaweza kuwa na faida au hasara, kwa kile walichokifanya, mimi na wasanii wote bila kujali wa muziki au wa filamu tuwaombee kwa vyombo vyote husika kwa kuwa natumaini wamejifunza na naomba tu wapewe dhamana”.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad