TCRA Yataka Wateja wa DSTV, AZAM na ZUKU Waliolipishwa Kuwasilisha Taarifa Zao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

TCRA Yataka Wateja wa DSTV, AZAM na ZUKU Waliolipishwa Kuwasilisha Taarifa Zao
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imewataka wateja visimbuzi vya DSTV, ZUKU na AZAM kutuma taarifa zao zinazoonesha na kuthibitisha kuwa wamekuwa wakilipia chaneli za ndani jambo ambalo ni kinyume na sheria.

TCRA imewataka wateja wa ving’amuzi hivyo kutoa taarifa juu ya majina yao kamili yaliyosajiliwa katika king’amuzi, aina ya king’amuzi anachotumia, namba ya kadi ya king’amuzi chake, eneo alipo, kiasi cha pesa ambacho amekuwa akilipia kutazama chaneli hizo na idadi ya miezi aliyolipia.

Taarifa hiyo ni maalumu kwa mtazamaji aliyekuwa anatozwa kutazama chaneli za televisheni ya TBC 1, ITV, STAR TV, CHANNEL TEN, EAST AFRIKA TV, na CLOUDS TV.

TCRA imewataka wahanga hao kutoa taarifa hizo ofisini kwao kupitia barua pepe au barua ya kawaida kwenye anuani yao ya dg@tcra.go.tz au kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano kwa sanduku la Posta 474.

Mnamo Agosti 7, 2018 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania iliziamuru Kampuni za DSTV, AZAM TV na ZUKU kuondoa cheneli za kutazamwa bila kulipia baada ya kukiuka sheria na masharti ya leseni zao kwa kuwatoza watazamaji ada za viwango mbalimbali kutazama chaneli hizo ambazo kisheria zinapaswa kutazwa bure.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad