AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mbunge wa Tarime Vijijini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, amelalamikia hatua ya jeshi polisi wilayani bariadi kuzuia mkutano wa ndani wa chama hicho ambao ulilenga kutoa mafunzo kwa wanachama wake kuelekea uchaguzi.
Kwa mujibu John Heche amesema chama hicho kinaendesha mafunzo kwa wanachama wake ambao wataenda kusimamia suala la uchaguzi kwenye ngazi ya msingi hivyo wamehuzunishwa na jeshi la polisi kuzuia mkutano wao licha ya kuwa wameshatumia gharama kuandaa.
"Sisi tuna uchaguzi ndani ya chama chetu kwa hiyo tunatoa mafunzo kwa viongozi wetu wa kanda mbili za Viktoria na kanda Serengeti ni jinsi gani wanaenda kutoa mafunzo ya kusimamia uchaguzi wilayani, lakini ghafla watu wetu wa mafunzo wamefika wamezuiliwa." Amesema John Heche
"Mkuu wa wilaya kaitisha mkutano, kasema haitaki kuiona CHADEMA wilayani kwake, lakini jana akaenda kukamata baadhi ya wanachama wetu waliokuwa wamelala lodge pamoja na wamiliki kwa sababu gani wameruhusu wanachama wetu kulala kwenye lodge, lakini kiujumla ni vikao vya ndani ambavyo Rais ameruhusu." Ameongeza John Heche.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK