Kijana wa Miaka 28 Amuua Baba Yake Mzazi Baada ya Kunyima Hela ya Mahali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kijana wa Miaka 28 Amuua Baba Yake Mzazi  Baada ya Kunyima Hela ya Mahali
Jeshi la Polisi mashariki mwa mji wa Eldoret, kaunti ya Uasin-Gishu magharibi mwa Kenya imemkamata mwanaume mwenye umri wa miaka 28, Andrew Kimutai, akituhumiwa kumuua baba yake, Joseph Marindany .


Akithibitisha tukio hilo OCPD wa Eldoret Mashariki Bw Richard Omanga, amesema kuwa Andrew anatuhumiwa kumuua baba yake kwa kumkata kichwa kwa kutumia shoka, baada ya kukataa kumpa kondoo wa familia ili alipe mahari kukomboa mtoto wake wa kiume aliyempata nje ya ndoa.

“Marehemu alikataa kumpa mwanawe kondoo kwa sababu hakujua alikuwa amezaa mtoto nje ya ndoa kama alivyodai. Mshukiwa alikasirishwa na msimamo wa baba yake ndipo alimvamia baba yake akiwa chumbani mwendo wa saa moja, akamkatakata kwa shoka,” alisema OCPD Omanga.

Mtuhumiwa huyo kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Naiberi akisubiri kufunguliwa mashtaka baada ya uchunguzi kukamilika.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad