AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres sasa anasema kuwa ''anataka ukweli'' kuhusiana na kutoweka kwa mwanahabari Jamal Khashoggi.
Bwana Guterres ameimbia BBC kuwa anahofia visa vya kutoweka kwa watu kama vile mwanahabari Jamal Khashoggi huenda ikawa "Jambo la kawaida''.
Khashoggi, ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya Saudi Arabia alitoweka Oktoba 2 katika mazingira ya kutatanisha baada ya kutembelea ubalozi wa nchi hiyo mjini Istanbul, Uturuki.
Mwanamfalme Mohammed bin Salman amekosolewa kuhusiana na kutoweka kwa mwanahabari Jamal Khashoggi
Saudi Arabia imekanusha madai kwamba ilitoa amri ya kuawa kwa mwanahabari ikisema madai hayo ni ya "uwongo".
Waziri wa uslama wa kitaifa ya wa Saudi Arabia, mwana mfalme Abdulaziz bin Saud bin Naif bin Abdulaziz, amenukuliwa na shirika la habari la Saudia akisema kuwa ufalme huo pia unataka kubaini ukweli kuhusiana na kisa cha kutoweka kwa mwanahabari Khashoggi.
Vianzo vya habari kutoka idara ya usalama nchi Uturuki vimeiambia BBC kwamba maafisa nchini wana kanda ya sauti na video kuthibitisha kuwa bwana Khashoggi aliuawa ndani ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Istanbul.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK