AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ariana Grande ameweza kushikilia chart za Billboard 200 kwa kushika nafasi ya kwanza mara tatu ikiwemo na album yake ya ‘Sweetner’ ambayo ilikaa nafasi ya kwanza mwezi wa August 2018 na kushika rekodi ya kuwa msanii wa nne wa kike kuingiza nyimbo nyingi kwenye chart za Billboard Hot 100.
Mkuu wa maudhui ya Billboard Ross Scarano amesema kuwa Ariana Grande anastahili kupata tuzo hiyo kutokana na kutoa aina ya muziki ambao jamii inanufaika nao ikiwa na kujiamini na kusimama peke yake. Ugawaji wa tuzo hizo unatarajiwa kufanyika usiku wa December 6,2018 katika sherehe za Woman In Music jijini New York.
Ariana Grande ataungana na wakali kama Selena Gomez, Madonna, Lady Gaga na Taylor Swift ambao pia waliwahi kukabidhiwa tuzo hiyo kutokana na mchango mkubwa wa muziki wanaoufanya.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK