CCM Yafunga Rasmi Pazia la Kuwapokea Wabunge na Madiwani Toka Upinzani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza rasmi kufunga pazia la kuwapokea viongozi, wabunge na madiwani wanaohamia chama hicho kutoka upinzani.


Akitangaza kufungwa kwa suala hilo jana mjini Morogoro, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula, alisema leo ndio mwisho wa kupokea viongozi, madiwani na wabunge kutoka vyama vya upinzani na kwamba atakayetaka kujiunga na chama hicho baada ya hapo atakuwa mwanachama wa kawaida.


“Huu ni uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM kwamba ifikapo Novemba 15 iwe mwisho wa kupokea viongozi, madiwani na wabunge kutoka upinzani, hivyo leo nimefunga rasmi jambo hili. Baada ya hapo, atakayetaka kurudi atabaki kuwa mwanachama wa kawaida,” alisema.


Wakati akitangaza hilo jana, tangu kuanza kwa hamahama ya wabunge na madiwani wa upinzani, CCM imeshapokea zaidi ya wabunge na madiwani 150 ambao pamoja na kujiengua upinzani, waliteuliwa na CCM kugombea nafasi zao na kushinda.


Wabunge waliojiuzulu nyadhifa zao kutoka upinzani ni Pauline Gekul (Babati Mjini), Mwita Waitara (Ukonga), Joseph Mkundi (Ukerewe), James ole Millya (Simanjiro), Dk. Godwin Mollel (Siha), Julius Kalanga (Monduli) na Chacha Ryoba (Serengeti) wote kutoka Chadema, Zuberi Kachauka na Maulid Mtulia (kutoka CUF).


Mbali na wabunge hao, wengine ambao walijiengua upinzani ni pamoja Anna Mghwira, aliyekuwa mgombea urais kupitia ACT-Wazalendo ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.


Wengine ni Profesa Kitilla Mkumbo ambaye sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, David Kafulila, Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe na aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patroba Katambi, sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma.


Viongozi hao, wakiwamo wabunge, wakati wa kutangaza uamuzi wao wa kujiunga na CCM walisema wamefanya hivyo, ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya Rais John Magufuli katika kuwaletea maendeleo wananchi.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad