AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Buheti amefunguka hayo baada ya kuibuka kwa kauli ya msanii mwenzake, Zuwena Mohammed 'Shilole' akisema kuwa yeye ndiye msanii wa kwanza kuanza kufanya biashara ya chakula, na hao wengine wamemuiga hivyo wasipokuwa na msingi imara wataanguka.
Akizungumza na www.eatv.tv, Buheti ameeleza kuwa alikuwa akichukua tenda za chakula kutoka kwa watu mbalimbali kupitia ukurasa wake wa instagram, lakini pia alitengeneza futari wakati wa ramadhani.
''Nilianza biashara ya chakula tangu 2016, nilikuwa na 'post' instagram kwamba kesho ntapika chakula fulani kwa hiyo napokea 'order' zenu, baaada ya hapo unapigiwa simu, nawapikia vyakula vyao halafu wanapelekewa," amesema Buheti.
"Lakini baadae nikasema kwanini nisifungue sehemu yangu, ndiyo nikaamua kufata sheria zote na kuanzisha eneo langu,'' ameongeza.
Msanii huyo pia amewaomba wasanii wenzake wawe na upendo, lakini pia wafanye kazi kwa bidii kwani ndio jinsi pekee ya kufanikiwa.
''Watu wakunjue nafsi zao na kupendana kiukweli, lakini pia watu wafanye kazi na kuacha kuongeongea kwasababu huu ni mwaka wa vitendo''.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK