AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza kwenye ibada takatifu iliyofanyika kanisa la Mtakatifu Immaculata Kurasini Jijini Dar es salaam, Rais Magufuli amesema Askofu Chengula alikuwa moja ya viongozi wa dini wa mfano waliopinga hadharani vitendo vya mapenzi ya jinsia moja.
“Askofu Chengula ameitangaza injili kwelikweli, hakusita kuzungumza ukweli na hivi karibuni alizungumza na kupinga hadharani kuhusu ushoga, ni viongozi wachache wanaoweza kupinga hadharani maovu yaliyokatazwa kwenye biblia.”
“Kwa nafasi hii nawapa pole sana waumini wa Kanisa Katoliki na watu wake wa Jimbo la Mbeya, na Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi amina,” ameongeza Rais Magufuli.
Novemba 21 mwaka huu Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mbeya, Evarist Chengula alifariki dunia majira asubuhi akiwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alipokuwa anapatiwa matibabu ya moyo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK