AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kassim Majaliwa ametoa agizo hilo mapema leo, kwenye mkutano wa hadhara wilayani hapo ambapo yupo katika ziara ya kikazi, na kubainisha kuwa tayari watu 7 wameshakamatwa akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo.
''Nimefika hapa, tumefanya vikao na viongozi wa halmashauri na tumebaini ubadhilifu wa fedha za miradi mbalimbali hivyo nimeagiza wahusika wote wakamatwe akiwemo mkaguzi wa ndani ambaye hajahudhuria kikao'', amesema Majaliwa.
Watumishi hao wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale akiwemo Mkurugenzi wanatuhumiwa kwa ubadhilifu wa fedha zaidi ya shilingi bilioni tatu, fedha ambazo zilitolewa na Serikali kwaajili ya kukamilisha miradi ya maendeleo.
Mbali na hilo Waziri Mkuu amewaonya wanaume wa mkoani Geita kwa ujumla juu ya suala la kuwapa mimba wanafunzi na kusema atakayekutwa amesimama na binti katika kona isiyoeleweka atakamatwa na kwenda kutumikia adhabu ya miaka 30 jela.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK