Moyo Wasahaulika Ndani ya ndege

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Inaripotiwa kuwa ndege hiyo ilikuwa imepaa angani kwa karibu saa tatu

Ndege ya abiria ya Marekani iliyokuwa ikisafiri kutoka mji wa Seattle kuenda Dallas ililazimika kukatiza safari baada ya moyo wa binadamu kusahaulika ndani yake.

Shirika la ndege la Southwest linasema kuwa kiungo hicho kilisafirishwa Seattle kutoka California, ambako ilitarajiwa kutolewa mishipa ambayo ingetumiwa baadaye kwa utaratibu wa tiba ya upandikizaji.

Lakini kisanduku ambacho kilikuwa kimehifadhi moyo huo kilisahaulika ndani ya ndege hiyo na hilo lilifahamika baada ya ndege kuanza safari kuelekea Dallas.

Kisa hicho kilitokea siku ya Jumapili lakini kiliangaziwa katika vyombo vya habari siku ya Alhamisi.

Abiria waliyokuwa ndani ya ndege hiyo wanasemakana kushutuka sana wakata rubani alipowaambia kuhusiana na mzigo huo na kwamba hana budi kugeuza mkondo na kurejea walikotoka.

Baadhi yao walitumia simu zao kujifahamisha kuhusu muda ambao moyo unaweza kuhifadhiwa kabla ya itumike kwa upasuaji- kwa mujiu wa wataalamu, moyo wa binadamu huchukuwa kati ya saa nne na sita kuharibika.

Ndege hiyo iliripotiwa kupaa angani kwa karibu saa tatu.

Daktrai mmoja aliyekuwa miongoni mwa wasafiri na ambaye hakuwa na uhusiano wowote wa kusafirisha kiungo hicho aliiambia gazeti la Seattle Times, kwamba tukio hilo ni ''utepetevu wa hali ya juu''.

Baada ya ndege hiyo kutua salama mjini Seattle, moyo huo ulipelekwa katika kituo cha afya cha kuhifadhiwa.

Gazeti hilo liliongeza kuwa kiungo hicho kilipokelewa na kuhifadhiwa katika muda uliyostahili
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad