AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mmoja wa wabunge ambaye amechochea hoja hiyo Abdifitah Ismail Dahir ameiambia BBC wanamtuhumu Rais kwa uhaini baada ya kusaini makubaliano ya kisiasa na kiuchumi na Ethiopia na Eritrea.
Amesema Rais ameshindwa kuwashirikisha taarifa wenzie kuhusiana na makubaliano yanayohusisha bandari za Somalia.
Wanamlaumu pia Rais kwa madai ya kuwarejesha wahalifu isivyo halali.
Wabunge wapatao 92 wanapaswa kusaini hoja hiyo ya kutokuwa na imani na Rais, kuweza kuwasilisha kwa Spika, ili aruhusu kuanza kwa mjadala.
Mizozo ya kisiasa ni jambo la kawaida nchini Somalia na utata huo wa hivi karibuni umekuja wakati serikali ikikosolewa kwa kuingilia kati uchaguzi wa majimbo.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK