Zitto Kabwe Aeleza Hofu Yake Baada ya Kutoka Takukuru

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Zitto Kabwe Aeleza Hofu Yake Baada ya Kutoka Takukuru
Kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, amesema ana hofu kuwa maelezo yake aliyoyatoa TAKUKURU yanaweza yasitumike kusaidia kuondoa tatizo la rushwa.

Zitto ameweka wazi hilo baada ya kutoka kufanya mahojiano na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),  ambayo ilimuita baada ya kutoa madai kuwa kuna rushwa inafanyika kwenye uagizaji wa bidhaa za chuma nje ya nchi.

''Nimewaeleza tangu mwanzo kuwa nina wasiwasi, pamoja na kwamba wamekuwa wakitimiza wajibu wao kitu ambacho ni jambo zuri lakini hofu yangu ni kwamba isije ikawa kuniita kwao ni kujaribu kuzima jambo hili na sio kufuatilia'', alisema Zitto.

Aidha Zitto amesema amewapa changamoto TAKUKURU ya kushughulikia malalamiko ambayo yapo ya uagizwaji wa bidhaa za chuma nje ya nchi wakati kuna viwanda vinazalisha hapa nchini.

Disemba 1, 2018, TAKUKURU ilimuita Zitto kwa lengo la kutaka kudhibitisha madai yake ya uwepo wa kampuni tatu za Chuma kutoka China, Urusi na Uturuki ambazo zimewahonga watendaji wa Wizara za Fedha na Viwanda pamoja na Ofisi ya Rais kwaajili ya kuchelewesha mradi wa Mchuchuma na Liganga.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad