AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mafanikio ni jambo ambalo kila mmoja wetu analitamani katika maisha yake, hivyo ili tuweze kufanikiwa zaidi katika maisha haya zipo tabia za watu wenye mafanikio ambao huzifanya, hivyo na sisi kama tutaamua kuzifanya tabia hizo basi mafanikio makubwa yatakuwa upande wetu.
Zifutazo ndizo tabia za watu wenye mafanikio:
Mara nyingi watu wenye mafanikio huwa mtazamo chanya, wao huangalia mafanikio katika picha kubwa. Kama anataka kufanya biashara huangalia biashara hiyo kwa picha ya miaka ijayo na si kuangalia picha ya biashara hiyo kwa wakati uliopo tu.
Mara nyingi watu wenye mafanikio hutafuta njia sahihi itakayowasaidia wao ili waweze kufika katika mafanikio makubwa zaidi ya hapo walipo sasa.
Watu wenye mafanikio hujua wanataka nini haswa, hivyo hujikita zaidi kwa yale wanayoyataka na si vinginevyo.
Watu wenye mafanikio ni watu wa kuchukua hatua zaidi kwa kile ambacho huona ni bora zaidi kwao, wao huongozwa na vitendo zaidi dhidi ya maneno katika kutekeleza mambo yao mbalimbali.
Hushughulika zaidi na malengo waliyoyapanga kufanya. Mambo ambayo hawakuyapanga kufanya huwa wanaachana nayo.
Kwa kila changamoto ambayo inawakabili katika maisha yao huwa hawazichi changamoto hizo ziendelee kuwa kikwazo bali huwa wanatafuta majibu sahihi kwa kila changamoto hizo.
Nguvu zao nyingi huwekeza katika kujifunza mambo mapya kila siku na kila wakati.
Hivyo ndugu yako kufanikiwa kwako inawezekana kabisa endapo utaamua kuiga tabia hizo za watu waliofanikiwa katika maisha yao.
Endelea kutembelea Muungwana Blog kila wakati.
Na. Benson Chonya
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Nadhani inategemea zaidi na maana ya neno "mafanikio" ...hebu angalia huyu rais wa Marekani sasa !!!!! Ana mafanikio au hana?
ReplyDelete