AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Maradona, hivi karibuni alitengana na Rocio Oliva, 28, na alikuwa amemzidi miaka 30 mrembo huyo.
Akizungumza na kituo kimoja cha redio nchini Argentina, Maradona alisema: “Mimi siyo mpigaji wa mke, lakini yule nilitaka kumkata kichwa.
“Alisaini makubaliano kwamba hatazungumza chochote. Hizo bata anazokula kwenye mapumziko yake, anafanya hivyo kwa pesa zangu. Sasa yupo nje kabisa ya maisha yangu.”
Wawili hao walimwagana hivi karibuni, baada ya miaka sita pamoja. Maradona amesema ataichukua nyumba aliyompa mrembo huyo jijini Buenos Aires.
“Nyumba niliyowapa familia yake ni yangu, nakwenda kuichukua. Samahani kama hawajui kumtunza mtoto wao. Mimi siyo Father Krismasi ambaye nazunguka mtaani kuwauliza watu wanahitaji nini. Nafanya kazi kama mtu yeyote yule duniani anavyofanya.”
Maradona aliongeza kuwa Oliva hayupo vizuri kichwani, na penzi lao limekufa.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK